Back to results

The Open University of Tanzania

Kutathmini Mila na Desturi za Mwanamke wa Visiwani katika Tenzi za Howani na Mwana Kukuwa

Abstract

dc:description.abstract

Diwani ya Howani Mwana Howani ni Diwani ambayo imekusanya tenzi mbili ambazo ni Howani na Mwana Kukuwa.Tenzi hizo zinazungumzia mila na desturi za Mwanamke wa Visiwani kuanzia alipobeba ujauzito mpaka alipoolewa na kupelekwa kwake. Hivyo katika utafiti huu mtafiti alichunguza vipengele vya fani kama vile: matumizi ya lugha, mandhari na wahusika ili kuona ni jinsi gani mila na desturi za mwanamke wa visiwani zilivyojidhihirisha katika tenzi teule. Utafiti huu ulitumia mbinu ya maktabani. Data zilikusanywa kwa kutumia mbinu ya usomaji makini na upitiaji wa nyaraka. Wateuliwa wa utafiti huu waliteuliwa kwa kutumia mbinu ya uteuzi lengwa. Aidha, data zilizokusanywa katika utafiti huu, zilichambuliwa kwa kutumia mbinu ya kimaelezo. Utafiti huu umegunduwa kuwa tenzi za Howani na Mwana Kukuwa zimejedili kwa kiasi kikubwa mila na desturi za mwanamke wa visiwani. Mila na desturi hizo zimeanzia tokea mwanamke alipokuwa mja mzito, kipindi cha kujifunguwa, malezi ya mtoto wa kike, kipindi cha kubaleghe, kipindi cha ndoa, katika mavazi, mapambo, ngoma za asili, pamoja na tiba za asili. Utafiti huu umeongozwa na Nadharia ya Sosholojia katika kuelezea lengo mahsusi la kwanza na la pili na Nadharia ya Semiotiki imetumika katika kuchambua data zinazohusiana na lengo mahsusi la tatu, ili kufikia lengo la utafiti huu. Matokeo ya utafiti huu yanaonesha kuwa vipengele kama vile mandhari, matumizi ya lugha pamoja na wahusika vimejitokeza kwa kiasi kikubwa katika tenzi za Howani na Mwana Kukuwa, vipengele hivyo vimesaidia sana katika kufikisha malengo ya Mwandishi ya kuelezea Mila na Desturi za mwanamke katika jamii ya visiwani Zanzibar.

Degree

thesis:*
Level dc:type.qualificationlevel
masters
Grantor dc:publisher.institution
The Open University of Tanzania
Year dc:date.issued
2016

Author and committee

dc:creator, dc:contributor.*
Author dc:creator
  • Mohamed, Fatma Ali

Subjects

dc:subject × 1

Rights

Language dc:language
en

Chain of custody

source
Harvested from
Open University of Tanzania
Base URL
repository.out.ac.tz/cgi/oai2
Last updated
2026-07-24
Source record
OAI-PMH GetRecord
citation

Mohamed, Fatma Ali. Kutathmini Mila na Desturi za Mwanamke wa Visiwani katika Tenzi za Howani na Mwana Kukuwa. masters thesis, The Open University of Tanzania, 2016.