Back to results

The Open University of Tanzania

Mtindo katika Riwaya ya Marimba ya Majaliwa ya Edwin Semzaba

Abstract

dc:description.abstract

Lengo kuu la utafiti huu lilikuwa ni kuchambua matumizi ya mtindo katika riwaya ya Marimba ya Majaliwa. Malengo mahususi yalikuwa mawili ambayo ni kuchambua matumizi ya mtindo yanayohusiana na lugha katika riwaya ya Marimba ya Majaliwa na kubainisha matumizi ya mtindo yanayohusiana na vipengele vinginevyo vya kimtindo katika riwaya ya Marimba ya Majaliwa. Data za utafiti zimekusanywa kwa kutumia mbinu za usomaji makini na upitiaji wa nyaraka. Data hizo zilizokusanywa zilichambuliwa kwa kutumia mkabala wa kimaelezo na nadharia ya Simiotiki. Kwa upande wa lengo mahususi la kwanza, matokeo ya utafiti yanabainisha kuwa matumizi ya kimtindo ya lugha ni pamoja na tamathali za usemi za tashibiha, chuku na takriri. Pia kuna matumizi ya methali na Kiswahili cha kimaeneo. Kwa upande wa lengo mahususi la pili, matokeo ya utafiti ni kuwa vipengele vingine vya kimtindo vilivyotumika katika riwaya teule ni matumizi ya nyimbo, hadithi ndani ya hadithi, mwingiliano matini, tanzu ndani ya tanzu ndani ya tanzu na uhalisia mazingaombwe.

Degree

thesis:*
Level dc:type.qualificationlevel
masters
Grantor dc:publisher.institution
The Open University of Tanzania
Year dc:date.issued
2016

Author and committee

dc:creator, dc:contributor.*
Author dc:creator
  • Silavwe, Martha Isaack

Subjects

dc:subject × 1

Rights

Language dc:language
en

Chain of custody

source
Harvested from
Open University of Tanzania
Base URL
repository.out.ac.tz/cgi/oai2
Last updated
2026-07-24
Source record
OAI-PMH GetRecord
citation

Silavwe, Martha Isaack. Mtindo katika Riwaya ya Marimba ya Majaliwa ya Edwin Semzaba. masters thesis, The Open University of Tanzania, 2016.