Back to results

The Open University of Tanzania

Dhima ya Ufutuhi Katika Riwaya za Shaabani Robert

Abstract

dc:description.abstract

Tasnifu hii imejaribu kuchangia mawazo na fikra za jinsi ya kutumia fasihi ya lugha katika kufikisha ujumbe uliokusudiwa kupitiya fani ya ufutuhi. Dhima ya ufutuhi katika Riwaya za Shaaban Robert imeathiri wasomaji, watunzi na wapenzi wa lugha ya Kiswahili kwa kiwango cha juu sana. Sura ya kwanza inatoa utangulizi wa ujumla historia ya marehemu Shaaban Robert, maisha yake, familia yake, kazi na ajira zake, mbari zake kwa ujumla na kazi zake za fasihi alizofanya. Sura ya pili inaelezea mawanda yakinadharia, mkabala wakinadharia ambao umetoa mchango katika kazi hii yaani nadharia tete na nadharia kiongozi. Sura ya tatu ni tahakiki za kazi mbalimbali zilizotangulia ikielezea kazi mbalimbali kuhusu ufutuhi na Dhima ya ufutuhi pamoja na maudhui yake katika Riwaya zilizo lengwa. Sura ya nne inafafanua mbinu za utafiti ambazo zimetumika ikiwa ni pamoja na umakinifu, usaili na hojaji. Sura ya tano imewasilisha matokeo ya utafiti. Yanaonesha kuwa uhai wa fasihi ya Lugha unategemea ufundi na umakini wa mpangilio wa maneno. Kiini ikiwa ni dhima ya ufutuhi ili kufikisha ujumbe uliokusudiwa. Kutokana na kukua kwa lugha ya Kiswahili na uwanda wake mpana wa fasihi imeonesha wazi kuwa, Dhima ya ufutuhi ni muhimu sana katika fasihi ili kuamsha ari na kuleta mvuto wa Lugha ya Kiswahili hususani katika kizazi hiki kilichopo. Hatimaye ni hitimishi na mapendekezo yaliyotolewa kama vile kuhimiza misingi bora ya ufundishaji wa Lugha ya Kiswahili, mbinu shirikishi za dhima ya ufutuhi kulingana na wakati uliopo na kuhamasisha jamii na Taifa letu kuipenda na kuithamini lugha ya Kiswahili kama Lugha ya Taifa. Kusoma vitabu vyake Shaaban Robert, kuzuru maeneo ya asili yake na kuviingiza vitabu vyake katika mtalaa wa Elimu na somo la Kiswahili kwa ngazi zinazohusika.

Degree

thesis:*
Level dc:type.qualificationlevel
masters
Grantor dc:publisher.institution
The Open University of Tanzania
Year dc:date.issued
2013

Author and committee

dc:creator, dc:contributor.*
Author dc:creator
  • Kabeja, Fortunata Moses

Subjects

dc:subject × 1

Rights

Language dc:language
en

Chain of custody

source
Harvested from
Open University of Tanzania
Base URL
repository.out.ac.tz/cgi/oai2
Last updated
2026-07-24
Source record
OAI-PMH GetRecord
citation

Kabeja, Fortunata Moses. Dhima ya Ufutuhi Katika Riwaya za Shaabani Robert. masters thesis, The Open University of Tanzania, 2013.