Back to results

The Open University of Tanzania

Kutathmini Nafasi ya Mwanamke katika Mashairi ya Kiswahili: Uchunguzi wa Mashairi ya Shaaban Robert na Mathias Mnyampala

Abstract

dc:description.abstract

Mada ya utafiti huu ni “Kutathmini Nafasi ya Mwanamke katika Mashairi ya Kiswahili: Uchunguzi wa Mashairi ya Shaaban Robert na Mathias Mnyampala.” Lengo kuu la utafiti huu lilikuwa ni kulinganisha nafasi ya mwanamke katika mashairi ya Shaaban Robert na Mathias Mnyampala ili kubaini falsafa yao juu ya mwanamke katika jamii. Madhumuni mahususi ya utafiti huu yalikuwa ni kulinganisha na kulinganua usawiri wa mwanamke katika mashairi ya Shaaban Robert na Mathias Mnyampala, kulinganisha na kulinganua matumizi ya lugha ya kisanaa inayotumiwa na Shaaban Robert na Mathias Mnyampala katika kusawiri nafasi ya mwanamke na kubainisha falsafa ya Shaaban Robert na Mathias Mnyampala juu ya nafasi waliyompa mwanamke katika mashairi yao. Nadharia ya Kifeministi ndiyo iliyotumika katika uchambuzi wa data za utafiti huu. Mbinu za usaili, hojaji na usomaji makini ndizo zilizotumika katika kukusanya data za utafiti. Matokeo ya utafiti yanaonesha kuwa mwanamke anasawiriwa kama chombo cha starehe kwa mwanaume, mwanamke ni kiumbe mpole na mnyenyekevu kwa mumewe, ni mama na mlezi katika jamii, mwanamke na suala la uaminifu na mwanamke na suala la umalaya na uasherati. Matumizi ya lugha ya tamathali za takriri, tashibiha, taswira na ishara ndizo zilizotumika kusawiri nafasi ya mwanamke katika mashairi yaliyotafitiwa. Falsafa yao juu ya mwanamke inasema, mwanamke ni kiumbe mwenye daraja ya juu katika malezi na ustawi wa jamii nzima na si familiya yake tu.

Degree

thesis:*
Level dc:type.qualificationlevel
masters
Grantor dc:publisher.institution
The Open University of Tanzania
Year dc:date.issued
2014

Author and committee

dc:creator, dc:contributor.*
Author dc:creator
  • Ali, Ali Edris

Subjects

dc:subject × 1

Rights

Language dc:language
en

Chain of custody

source
Harvested from
Open University of Tanzania
Base URL
repository.out.ac.tz/cgi/oai2
Last updated
2026-07-24
Source record
OAI-PMH GetRecord
citation

Ali, Ali Edris. Kutathmini Nafasi ya Mwanamke katika Mashairi ya Kiswahili: Uchunguzi wa Mashairi ya Shaaban Robert na Mathias Mnyampala. masters thesis, The Open University of Tanzania, 2014.