Back to results

The Open University of Tanzania

Kuchunguza fani na dhamira katika semi zilizoandikwa katika vyombo vya safari vya Baharini Kisiwani Pemba

Abstract

dc:description.abstract

Utafiti huu unalenga kuchunguza fani na dhamira katika semi za vyombo vya safari vya baharini kisiwani pemba semi hizo zinatumika katika shughuli za maisha ya wapemba ambapo zimeibua dhamira mbalimbali. Utafiti huu ulikua na malengo kama yafuatayo:lengo kuu la utafiti huu ni kuchukunguza fani na dhamira katika semi za vyombo vya safari vya baharini kisiwani pemba. Malengo mahasusi ni: 1. kubainisha semi katika vyombo vya safari vya baharini kisiwani Pemba 2. Kuonesha mbinu za kisanaa zilizotumika katika semi za vyombo vya safari vya baharini kisiwani Pemba 3. Kueleza dhamira zinazopatikana katika semi za vyombo vya safari vya baharini kisiwani Pemba.Utafiti huu umefanyika Tumbe wilaya ya Micheweni na Kojani wilaya ya Wete Mkoa wa Kaskazini Pemba. Mbinu zilizotumika katika kukusanya data ni mbinu ya uwandani na mbinu ya maktabani, njia zilizotumika ni mahojiano na uchunguzi makini. utafiti huu ulitumia sampuli ya wazee vijana na walimu wa somo la kiswahili shule za sekondari.Nadharia zilizotumika katika utafiti huu ni nadharia ya simiotiki na nadharia ya muitiko wa msomaji. Kwa ujumla matokeo ya utafiti huu yanaonyesha kuwa Wapemba wanazo semi zinazotumika katika vyombo vya baharini. Semi zilizoandikwa katika vyombo vya baharini, zimetumika mbinu mbalimbali za kisanaa, mbinu hizo ni pamoja na tashtiti,taswira, kejeli, methali, misemo,simo, sitiri na kadhalika. Pia mtafiti aligundua kuwa semi hizo zina dhamira mbalimbali.

Degree

thesis:*
Level dc:type.qualificationlevel
masters
Grantor dc:publisher.institution
The Open University of Tanzania
Year dc:date.issued
2016

Author and committee

dc:creator, dc:contributor.*
Author dc:creator
  • Juma, Nassor Hamad

Subjects

dc:subject × 1

Rights

Language dc:language
en

Chain of custody

source
Harvested from
Open University of Tanzania
Base URL
repository.out.ac.tz/cgi/oai2
Last updated
2026-07-24
Source record
OAI-PMH GetRecord
citation

Juma, Nassor Hamad. Kuchunguza fani na dhamira katika semi zilizoandikwa katika vyombo vya safari vya Baharini Kisiwani Pemba. masters thesis, The Open University of Tanzania, 2016.