Back to results

The Open University of Tanzania

Matatizo Wanayoyapata Wanafunzi Walibya katika Kujifunza Viambishi vya Njeo katika Lugha ya Kiswahili

Abstract

dc:description.abstract

Utafiti huu wa 'Matatizo Wanayopata Wanafunzi Walibya katika Kujifunza Viambishi vya Njeo katika Kiswahili' ni wa kwanza na wa aina yake katika ulimwengu wa lugha ya Kiswahili. Hii ni kwa sababu kwa mara ya kwanza sasa tunapata utafiti unaohusu baadhi ya matumizi yanayowakwamisha wanafunzi wengi kama vile Walibya kujifunza kurnudu lugha ya Kiswahili ipasavyo. Kama jina la utafiti linavyoashiria, utafiti huu umefanywa ili kuonyesha mojawapo ya matatizo yanayowakabili Wanafunzi Walibya wanaojifunza Kiswahili na kwa kiasi fulani walimu wanaowafundisha lugha hiyo. Nia hasa, ni kuonyesha undani wa tatizo hili na jinsi linavyoweza kutatuliwa ili kuwasaidia hasa wanafunzi kumudu vizuri masuala ya kisarufi ya Kiswahili Sanifu wakati wanajifunza. Ni dhahiri kwamba matokeo ya utafiti huu pia yatawasaidia walimu wanaowafundisha wanafunzi wenye asili ya Libya kuelewa misingi ya kisarufi ya lugha hii kwa haraka na kwa ufanisi. Maelezo haya yatafanywa katika sura tano kwa utaratibu ufuatao: Sura ya Kwanza itakuwa ni utangulizi unaoonyesha tatizo la utafiti, malengo ya utafiti, na mbinu zilizotumika katika utafiti. Sura hii pia inapitia maandishi mbalimbali hasa yale yaliyohusu viambishi vya njeo na kuweka nadharia tete za utafiti. Sura hii pia itatazama masuala ya kinadharia yanayohusiana na ufundishaji wa lugha ya pili. Sura ya Pili inachunguza kwa undani maumbile muhimu ya sarufi ya Kiswahili, hususani maumbo yanayojitokeza kuhusiana na viambishi vya njeo na maana zinazojitokeza zinazofanya matumizi yenye viambishi hivi kuwatatiza wanafunzi. Sura ya Tatu itatalii maumbile ya lugha ya Kiarabu na kubainisha athari zinazoweza kutokea kutokana na maumbo na mipangilio ya kisarufi katika lugha hii. Maelezo katika sura hii yatawasaidia walimu na wanafunzi kulinganisha masuala ya kisarufi baina ya lugha hizi wanazokabiliana nazo. Sura ya Nne itachanganua msingi ya matatizo ya viambishi vya njeo kwa wanafunzi wa Libya wanaojifunza Kiswahili. Sura ya tano itatoa hitimisho na mapendekezo mbalimbali.

Degree

thesis:*
Level dc:type.qualificationlevel
masters
Grantor dc:publisher.institution
The Open University of Tanzania
Year dc:date.issued
2010

Author and committee

dc:creator, dc:contributor.*
Author dc:creator
  • Mohammed, Jabir Alzarok Jabir

Subjects

dc:subject × 1

Rights

Language dc:language
en

Chain of custody

source
Harvested from
Open University of Tanzania
Base URL
repository.out.ac.tz/cgi/oai2
Last updated
2026-07-24
Source record
OAI-PMH GetRecord
citation

Mohammed, Jabir Alzarok Jabir. Matatizo Wanayoyapata Wanafunzi Walibya katika Kujifunza Viambishi vya Njeo katika Lugha ya Kiswahili. masters thesis, The Open University of Tanzania, 2010.