Back to results

The Open University of Tanzania

Maana za Majina ya Watu wa Pemba Katika Lugha ya Kiswahili: Uchunguzi Kifani

Abstract

dc:description.abstract

Utafiti huu ulichunguza maana za majina ya watu wa Pemba. Utafiti huu ulifanyika katika kisiwa cha Pemba mkoa wa kusini, Wilaya ya Chake-Chake. Mtafiti aliongozwa na malengo mahususi matatu. Kwanza, kubainisha maana za majina ya watu katika jamii ya Wapemba, pili kueleza mazingira yanayosababisha watu kupewa majina hayo katika jamii ya Wapemba na tatu kufafanua vigezo vinavyowaongoza watoa majina kwa wanaume na wanawake. Ili kufikia lengo kuu lililokusudiwa mbinu mbalimbali za utafiti zilihusika. Mbinu hizo ni pamoja na mahojiano na hojaji. Utafiti huu uliongozwa na nadharia ya semiotiki ambayo msingi wake mkubwa ni ishara na maana zake katika lugha. Nadharia ya pili iliyotumika ni nadharia jumuishi ya Giles ambayo msingi wake mkubwa ni kuchunguza vibainishi vya jamii mbalimbali. Nadharia hizi ziliakisi data za utafiti huu kutokana na maoni yaliyotolewa na watafitiwa. Utafiti umebaini kuwa majina yanayotolewa kwa watu yanabeba maana zifuatazo: Maana za majina yatokanayo na miezi ya kiislamu, matukio mbalimbali, maeneo matukufu, siku za wiki, miongo na hali mbalimbali walizozaliwa watoto. Mazingira yanayosababisha watu kutoa majina katika jamii ya Wapemba ni Siku wanazozaliwa watoto, wakati wanamozaliwa, miezi wanayozaliwa na migongano katika jamii. Utafiti umebaini vigezo vinavyowaongoza watoa majina kwa wanaume na wanawake kuwa ni Itikadi za kidini, urithi, umashuhuri, kuondokana na majina ya zamani na kuvutiwa na herufi fulani mwanzoni mwa jina na kuvutiwa na silabi fulani mwishoni mwa jina.

Degree

thesis:*
Level dc:type.qualificationlevel
masters
Grantor dc:publisher.institution
The Open University of Tanzania
Year dc:date.issued
2016

Author and committee

dc:creator, dc:contributor.*
Author dc:creator
  • Ali, Moh’d Haji

Subjects

dc:subject × 1

Rights

Language dc:language
en

Chain of custody

source
Harvested from
Open University of Tanzania
Base URL
repository.out.ac.tz/cgi/oai2
Last updated
2026-07-24
Source record
OAI-PMH GetRecord
citation

Ali, Moh’d Haji. Maana za Majina ya Watu wa Pemba Katika Lugha ya Kiswahili: Uchunguzi Kifani. masters thesis, The Open University of Tanzania, 2016.