Back to results

The Open University Of Tanzania

Haja ya lugha ya Kiswahili kutumika kufundishia elimu ya Sekondari.Mifano Kutoka Wilaya ya Ilemela-Mwanza

Abstract

dc:description.abstract

Utafiti huu ulikusudia kuchunguza haja ya lugha ya Kiswahili kutumika kufundishia elimu ya sekondari kwa kutumia mifano kutoka Wilaya ya Ilemela mkoani Mwanza. Lengo kuu la utafiti huu lilikuwa ni kuchunguza uhusiano baina ya kutotumika kwa Kiswahili katika ufundishaji wa masomo katika shule za sekondari na kushindwa kwa wanafunzi kupata maarifa yaliyokusudiwa. Utafiti huu ulikuwa na malengo mahsusi ambayo ni; Kubainisha mambo yanayo changia wanafunzi kukosa maarifa ya elimu ya sekondari, kubainisha athari zitokanazo na kutokutumika kwa lugha ya Kiswahili katika kufundishia elimu ya sekondari na kujadili changamoto zinazowakabili walimu na wanafunzi zitokanazo na kutotumika kwa Kiswahili katika ufundishaji wa elimu ya sekondari. Ili kufikia malengo hayo, utafiti huu ulitumia mbinu za maktaba, hojaji na dodoso. Nadharia iliyotumika kukusanya na kuchambua data za utafiti huu ni nadharia ya Matokeo ya utafiti huu yanadhihirisha kuwa, walimu na wanafunzi wanapendelea elimu ya sekondari itolewe kwa lugha ya Kiswahili badala ya kutumia lugha ya kigeni. Utafiti umedhihirisha kuwa, utolewaji wa elimu ya sekondari kwa lugha ya kigeni hauna mafanikio makubwa hata kama kauli mbiu ya sasa ya serikali ni matokeo makubwa sasa. Ni vigumu kupata matokeo makubwa ikiwa wanafunzi hawaelewa wanachofundishwa.Ili kupata matokeo makubwa na yenye ufanisi ni lazima serikali na wadau wote wa elimu waamue kukifanya kiswahili kuwa lugha ya kufundishia elimu ya sekondari.

Degree

thesis:*
Level dc:type.qualificationlevel
masters
Grantor dc:publisher.institution
The Open University Of Tanzania
Year dc:date.issued
2015

Author and committee

dc:creator, dc:contributor.*
Author dc:creator
  • Lunyana, Nicholaus Mvugamake

Subjects

dc:subject × 1

Rights

Language dc:language
en

Chain of custody

source
Harvested from
Open University of Tanzania
Base URL
repository.out.ac.tz/cgi/oai2
Last updated
2026-07-24
Source record
OAI-PMH GetRecord
citation

Lunyana, Nicholaus Mvugamake. Haja ya lugha ya Kiswahili kutumika kufundishia elimu ya Sekondari.Mifano Kutoka Wilaya ya Ilemela-Mwanza. masters thesis, The Open University Of Tanzania, 2015.