Back to search

The Open University of Tanzania

Kuchunguza Masuala ya Kisiasa Katika Riwaya za Shaaban Robert: Mfano wa Kusadikika na Kufikirika

Abstract

dc:description.abstract

Mada ya utafiti huu ilikuwa ni kuchunguza masuala ya Kisiasa katika Riwaya za Shaaban Robert: Mfano wa Kusadikika na Kufikirika. Lengo kuu la utafiti huu lilikuwa ni kutathimini masuala ya kisiasa katika riwaya za Shaaban Robert kupitia riwaya za Kusadikika na Kufikirika. Lengo kuu la utafiti huu limefikiwa baada ya madhumuni mahususi matatu kukamilika. Madhumuni hayo ni Kubainisha masuala ya kisiasa katika riwaya za Shaaban Robert, Kubainisha mchango wa Shaaban Robert katika maendeleo ya kisiasa nchini Tanzania na kuchunguza mbinu za kisanaa zinazotumiwa na Shaaban Robert kusawiri masuala ya kisiasa katika Kusadikika na Kufikirika. Data za utafiti huu zilikusanywa kwa kutumia mbinu za usaili na uchambuzi wa kimaudhui. Mikabala wa kidhamira na kimaelezo ndio iliyotumika kuchambua data za utafiti huu. Utafiti umebaini kuwa, masuala ya kisiasa yanayojitokeza katika riwaya za Kusadikika na Kufikirika ni uongozi mzuri, uongozi mbaya, utii wa sheria, masuala ya jinsia na kujifunza kutoka kwa wengine. Masuala haya yanawasilishwa na Shaaban Robert kwa kutumia mbinu za kisanaa za matumizi ya methali, misemo,tashibiha, kejeli, mandhari ya kidhanaishi na wahusika bapa. Masuala ya kisiasa yanayowasilishwa na Shaaban Robert yametoa mchango mkubwa katika kuimarisha uongozi wa nchi huru ya Tanganyika na baadae Tanzania.

Degree

thesis:*
Level dc:type.qualificationlevel
masters
Grantor dc:publisher.institution
The Open University of Tanzania
Year dc:date.issued
2014

Author and committee

dc:creator, dc:contributor.*
Author dc:creator
  • Massawe , Bibiana

Subjects

dc:subject × 1

Rights

Language dc:language
en

Chain of custody

source
Harvested from
Open University of Tanzania
Base URL
repository.out.ac.tz/cgi/oai2
Last updated
2026-07-24
Source record
OAI-PMH GetRecord
citation

Massawe , Bibiana. Kuchunguza Masuala ya Kisiasa Katika Riwaya za Shaaban Robert: Mfano wa Kusadikika na Kufikirika. masters thesis, The Open University of Tanzania, 2014.