Back to search

The Open University of Tanzania

Kuchunguza Dhamira za Nyimbo za Uganga Katika Jamii za Waswahili Wilaya ya Mkoani Kusini Pemba

Abstract

dc:description.abstract

Lengo kuu la utafiti huu lilikuwa ni kuchunguza dhamira za nyimbo za Uganga katika jammi za waswahili Wilaya ya Mkoani Kusini Pemba. Ili kutimiza lengo hili kuu tulikuwa na madhumuni mahususi matatu ambayo ni kubainisha dhamira zinazopatikana katika nyimbo za uganga, kufafanua undani wa dhamira za nyimbo za uganga zilimo katika jamii ya watu wa Kusini Pemba na kufafanua vipengele vya kifani vinavyosaidia kuibua dhamira zinazojitokeza katika nyimbo za uganga. Data za utafiti zimekusanywa kwa kutumia njia ya usaili na njia shirikishi katika maskanini. Data hizo zilikusanywa na kuchambuliwa kwa kutumia mkabala wa kimaelezo. Vile vile njia za kimaktaba zilitumika kwa mtafiti kwa ajili ya kujisomea kazi tangulizi na maandiko tafauti kwa lengo la kujiongezea maarifa na kufanikisha utafiti wake. Pia uchambuzi wa data ulifanywa kwa kutumia mkabala wa kinadharia. Nadharia zilizotumika ni Simiotiki na Mwitiko wa Msomaji. Ama kuhusu matokeo ya utafiti yanaonesha kuwa kwenye nyimbo za uganga kuna siri ambazo zimejificha na zilihitajika kuwekwa bayana na mtafiti. Kwa upande wa dhamira zilizojitokeza katika nyimbo za uganga zilitoa dhamira kama vile suala la Mmongonyoko wa Maadili, umoja na mshikamano, malezi, matabaka na kadhalika. Mwisho matfiti alitoa hitimisho, mapendekezo ya tafiti nyingine zifanyika katika muktadha wa uganga kwa kuangalia misamiati na njungu katika tiba ya uganga na kuiomba jamii yake iziendeleze tiba za asili katika fani ya uganga.

Degree

thesis:*
Level dc:type.qualificationlevel
masters
Grantor dc:publisher.institution
The Open University of Tanzania
Year dc:date.issued
2016

Author and committee

dc:creator, dc:contributor.*
Author dc:creator
  • Ali, Mussa Yussuf

Subjects

dc:subject × 1

Rights

Language dc:language
en

Chain of custody

source
Harvested from
Open University of Tanzania
Base URL
repository.out.ac.tz/cgi/oai2
Last updated
2026-07-24
Source record
OAI-PMH GetRecord
citation

Ali, Mussa Yussuf. Kuchunguza Dhamira za Nyimbo za Uganga Katika Jamii za Waswahili Wilaya ya Mkoani Kusini Pemba. masters thesis, The Open University of Tanzania, 2016.