Back to results

The Open University of Tanzania

Kuchunguza Vipengele vya fani katika Mashairi ya Kiswahili: Ulinganishi na ulinganuzi wa Mashairi ya Euphrase Kezilahabi na Haji Gora Haji

Abstract

dc:description.abstract

Utafiti huu ulikuwa na lengo kuu ambalo lilikuwa ni kuchunguza vipengele vya fani katika mashairi ya Kiswahili kwa kufanya ulinganishi na ulinganuzi wa mashairi ya Euphrase Kezilahabi na Haji Gora Haji. Lengo hili limejumuishwa katika utafiti huu ili kuweza kuona kama kuna kufanana na kutofautiana kwa vipengele vya kifani katika mashairi ya kisasa na yale ya kimapokeo. Vilevile, tukaona ni busara japo kwa ufupi kueleza ama kudokeza dhamira mbalimbali zinazowasilishwa katika aina hizi mbili za ushairi yaani ushairi wa kisasa na ule wa Kimapokeo. Ili kufanikisha malengo ya utafiti huu tumekusanya data kwa kutumia mbinu za maktabani na kufanya uwasilishaji na uchambuzi wa data kwa kuongozwa na mkabala wa kimaelezo kama inavyoonekana katika sura ya nne ya tasinifu hii. Matokeo ya utafiti yanaonesha kwamba, mashairi ya Euphrase Kezilahabi na yale ya Haji Gora Haji yanaonesha kutofautiana kwa vipengele vya kimuundo katika matumizi ya vina na mizani, kibwagizo, muundo wa tarbia katika beti za shairi zinatokeza sana katika ushairi wa Haji Gora Haji kuliko mashairi ya Euphrase Kezilahabi. Mashairi ya Euphrase Kezilahabi hayatumii kabisa vipengele hivi. Kwa upande wa kufanana kwao, tumeona kwamba, wote wawili wanatumia lugha ya mkato, taswira, wahusika pamoja na ucheshi. Vilevile, tumebaini kwamba Kezilahabi na Haji Gora Haji wanazungumza juu ya dhamira ambazo zinasawiri hali halisi ya maisha ya jamii ya Kitanzania na hata kwingineko duniani.

Degree

thesis:*
Level dc:type.qualificationlevel
masters
Grantor dc:publisher.institution
The Open University of Tanzania
Year dc:date.issued
2013

Author and committee

dc:creator, dc:contributor.*
Author dc:creator
  • Ali, Abdolha Mansour

Subjects

dc:subject × 1

Rights

Language dc:language
en

Chain of custody

source
Harvested from
Open University of Tanzania
Base URL
repository.out.ac.tz/cgi/oai2
Last updated
2026-07-24
Source record
OAI-PMH GetRecord
citation

Ali, Abdolha Mansour. Kuchunguza Vipengele vya fani katika Mashairi ya Kiswahili: Ulinganishi na ulinganuzi wa Mashairi ya Euphrase Kezilahabi na Haji Gora Haji. masters thesis, The Open University of Tanzania, 2013.