Back to results

The Open University of Tanzania

Kuchunguza Dhima ya Methali za Jamii ya Wasimbiti wa Rorya Mkoani Mara

Abstract

dc:description.abstract

Mada ya utafiti huu ilikuwa ni kuchunguza dhima ya methali za jamii ya Wasimbiti wa Rorya mkoani Mara. Ili kufanikisha mada hii utafiti ulikuwa na madhumuni mahususi matatu ambayo ni kubainisha dhima ya methali ya jamii ya Wasimbiti wa wilaya ya Rorya mkoani Mara, kuelezea uhalisia wa dhima za methali za jamii ya Wasimbiti kwa jamii ya leo na kubainisha mbinu za kisanaa zilizotumika kujenga dhima za methali za jamii ya Wasimbiti. Madhumuni haya matatu yamefanyiwa kazi na matokeo ya utafiti yamepatikana. Data za utafiti zilikusanywa kwa kutumia mbinu za usaili na upitiaji wa nyaraka na kuchambuliwa kwa kutumia mkabala wa kimaelezo na nadharia za Sosholojia na Simiotiki. Matokeo ya utafiti yanaonyesha kuwa methali za jamii ya Wasimbiti zina dhima za kuhamasisha jamii kuepuka tamaa , kuwa na subira, kuelimisha jamii juu ya maisha, kufanya kazi kwa juhudi na maarifa, kuhimiza umoja na mshikamano katika jamii na umuhimu wa malezi kwa vijana katika jamii. Pia, matokeo ya utafiti yanaonyesha kuwa methali za jamii ya Wasimbiti zinaundwa na mbinu za kisanaa za mafumbo, takriri, taswira na muundo. Mbinu hizi za kisanaa zimesaidia sana katika kuwasilisha dhima za methali za jamii ya Wasimbiti wanaoishi wilaya ya Rorya mkoani Mara.

Degree

thesis:*
Level dc:type.qualificationlevel
masters
Grantor dc:publisher.institution
The Open University of Tanzania
Year dc:date.issued
2016

Author and committee

dc:creator, dc:contributor.*
Author dc:creator
  • Sylvester, Angela Ghati

Subjects

dc:subject × 1

Rights

Language dc:language
en

Chain of custody

source
Harvested from
Open University of Tanzania
Base URL
repository.out.ac.tz/cgi/oai2
Last updated
2026-07-24
Source record
OAI-PMH GetRecord
citation

Sylvester, Angela Ghati. Kuchunguza Dhima ya Methali za Jamii ya Wasimbiti wa Rorya Mkoani Mara. masters thesis, The Open University of Tanzania, 2016.