Back to results

The Open University Of Tanzania

Ulinganishi wa kiisimu kati ya lahaja ya Kipemba na Kitumbatu

Abstract

dc:description.abstract

Kazi hii ilihusika na Ulinganishi wa Kiisimu uliopo baina ya lahaja ya Kipemba na Kitumbatu.Utafiti huu ulikuwa na malengo matatu ambayo ni kubainisha tofauti baina ya fonimu za Kipemba na Kitumbatu, kulinganisha na kutofautisha kanuni za kifonolojia na kimofofonolojia zinazotawala maumbo ya mofu zilizounda maneno ya Kipemba na Kitumbatu na kuainisha uwiano wa kimaana baina ya msamiati wa lahaja ya Kipemba na Kitumbatu. Ili kufikia lengo kuu lililokusudiwa mbinu mbalimbali za utafiti zilihusika, ambazo ni hojaji, mahojiano pamoja na ushuhudiaji. Nadharia mbili zilizoongoza utafiti huu ni nadharia ya fonolojia zalishi na nadharia ya lahaja na lahajia na Sampuli iliyotumika ni watu mia moja, hamsini kutoka Pemba na hamsini kutoka Tumbatu. Kwa upande wa matokeo ya utafiti, mtafiti aligundua kwamba, kifonolojia kuna utofauti mkubwa baina ya Kipemba na Kitumbatu, hasa kwenye idadi na aina za fonimu kwa upande mmoja na tofauti ya kimatumizi katika baadhi ya fonimu kwa upande wa pili. Pia imebainika kuwa, Kipemba na Kitumbatu kina tofauti kwenye baadhi ya viambishi nafsi za mtenda na mtendwa. Kanuni za Kifonolojia zinazobadilisha miundo ya ndani kuwa miundo ya nje ya maumbo ya vitenzi, nomino na hata baadhi ya vivumishi na viwakilishi zimetumika katika lahaja zote mbili, ingawa kitumbatu kimezidi kujikita kwenye matumizi ya kanuni nyingi zaidi kuliko Kipemba. Kipemba kimetofautiana na Kitumbatu kwenye msamiati mwingi hasa kwenye vitenzi na nomno. Lakini katika eneo hili Kipemba kipo karibu zaidi na Kiswahili Sanifu, wakati Kitumbatu kimejitenga mbali na Kiswahili Sanifu katika uwiano wa kimsamiati. Mtafiti amependekeza mambo kadha na kuwaagiza watafiti wajao wayatupie macho na kuyafanyia kazi. Miongoni mwa mapendekezo hayo ni pamoja na kufanya tafiti linganishi baina ya lahaja za Kiswahili, kufanya Ulinganishi wa Kiisimu baina ya Vipemba vizungumzwavyo ndani ya visiwa vidogo vidogo ndani ya Pemba.

Degree

thesis:*
Level dc:type.qualificationlevel
masters
Grantor dc:publisher.institution
The Open University Of Tanzania
Year dc:date.issued
2015

Author and committee

dc:creator, dc:contributor.*
Author dc:creator
  • Bakari, Bakari Kombo

Subjects

dc:subject × 1

Rights

Language dc:language
en

Chain of custody

source
Harvested from
Open University of Tanzania
Base URL
repository.out.ac.tz/cgi/oai2
Last updated
2026-07-24
Source record
OAI-PMH GetRecord
citation

Bakari, Bakari Kombo. Ulinganishi wa kiisimu kati ya lahaja ya Kipemba na Kitumbatu. masters thesis, The Open University Of Tanzania, 2015.