Back to results

The Open University Of Tanzania

Kuchunguza Ufasihi Simulizi unaojitokeza Ndani ya Hadithi za Kusadikika na Adili na Nduguze

Abstract

dc:description.abstract

Lengo la utafiti huu ni kuchunguza Ufasihi Simulizi unaojitokeza katika hadithi za Adili na Nduguze na Kusadikika za Shaaban Robert. Ili kukamilisha lengo hili, utafiti ulikuwa na malengo mahususi matatu ambayo ni; kufafanua vipengele vya fasihi simulizi vinavyojitokeza ndani ya hadithi za Kusadikika na Adili na Nduguze, kujadili mbinu zilizotumika katika kuhifadhi ufasihi simulizi uliomo ndani ya kazi husika, na kuelezea dhamira zinazojitokeza ndani ya hadithi za Kusadikika na Adili na Nduguze. Data za utafiti huu zimekusanywa kwa kutumia mbinu za usomaji makini na upitiaji wa nyaraka maktabani. Mkabala wa kimaelezo sambamba na nadharia za Mwitiko wa Msomaji na Ujumi ndizo zilizotumika katika kuchambua data za utafiti.Matokeo ya utafiti yamebaini kuwa fani za fasihi simulizi kama vile methali, misemo, hadithi ndani ya hadithi, nyimbo na masimulizi zimejitokeza kwa kiasi kikubwa katika kazi teule za Shaaban Robert. Vile vile, matokeo ya utafiti yanaonesha kuwa mbinu za kisanaa kama vile; muundo, mtindo, wahusika, mandhari na matumizi ya lugha zimetumika katika kuhifadhi ufasihi simulizi katika riwaya husika. Pia, matokeo ya utafiti yamegundua kuwa, katika kazi hizo kunajitokeza dhamira kama vile; umuhimu wa elimu, kilimo, uongozi bora, umuhimu wa sheria, mapenzi, choyo na husda, ndoa, malezi na kodi. Kwa ujumla, utafiti huu umegundua kuwa fasihi ni moja tu. Maandishi au Masimulizi ni namna za uwasilishaji wa fasihi ya Kiswahili na nyinginezo duniani. Aidha, utafiti umegundua kuwa, Fasihi ya Maandishi hutumia vipengele vile vile vya Fasihi ya Masimulizi ili kufikisha ujumbe kwa jamii. Hivyo, mpaka uliopo ni namna ya uwasilishaji wa kazi hizo

Degree

thesis:*
Level dc:type.qualificationlevel
masters
Grantor dc:publisher.institution
The Open University Of Tanzania
Year dc:date.issued
2015

Author and committee

dc:creator, dc:contributor.*
Author dc:creator
  • Salim, Muhammed Ali

Subjects

dc:subject × 1

Rights

Language dc:language
en

Chain of custody

source
Harvested from
Open University of Tanzania
Base URL
repository.out.ac.tz/cgi/oai2
Last updated
2026-07-24
Source record
OAI-PMH GetRecord
citation

Salim, Muhammed Ali. Kuchunguza Ufasihi Simulizi unaojitokeza Ndani ya Hadithi za Kusadikika na Adili na Nduguze. masters thesis, The Open University Of Tanzania, 2015.