Back to results

The Open University Of Tanzania

Kuchambuwa Maudhui ya Hadithi za Watoto Katika Jamii ya Wapemba

Abstract

dc:description.abstract

Kazi hii ilihusika na hadithi za Paukwa…. Pakawa. Imechunguza maudhui yanazopatikana katika hadithi za watoto katika jimbo la Mkanyageni Mkoa wa kusini Pemba. Ili kufikia lengokuu lililokusudiwa mbinu mbalimbali za utafiti zilihusika. Mbinu hizo ni za mahojiano pamoja na uchunguzi wa kimaktaba. Nadharia tatu za utafiti zilitumika. Nadhariza hizo ni mwitiko wa msomaji, nadharia ya simiotiki na nadharia ya sosholojia (kijamii).Kwa upande wa matokeo ya utafiti, mtafiti amegunduwa dhamira kadha wa kadha zilizoibuka kutokana na utafiti na uchambuzi alioufanya. Dhamira hizo ni ugumu wa upatikanaji wa elimu, umoja na mshikamano miongoni mwa wanajamii. mapenzi na ndoa, kuonya,nafasi ya mwanamke, ukarimu, uzembe na uvunjaji wa kanuni pamoja na utawala bora. Kifani, mtafiti amegundua kwamba, baadhi ya vipengele vya fani vilivyosaidia kuibua dhamira katika hadithi za watoto za Kipemba ni kipengele kinachohusu wahusika, matumizi ya lugha, muundo, mtindo na mandhari.Ujumbe uliojitokeza katika hadithi za watoto ni pamoja na wazee kuwaasa watoto juu ya kufuata ushauri wa wazazi wao kwa kila wanalotaka kulifanya, kujitenga na mambo mbalimbali ambayo yanaweza kukuletea vikwazo au matatizo, wanataalimu wawe wavumilivu, wasiwe na ufedhuli na lugha chafu kwa wanafunzi wao. Ujumbe mwengine uliopatikana ni kuwa na juhudi ya kazi na kuwacha kujigamba pasipo sababu, kutokuwa na imani na kila mtu,kuepuka ubinafsi na ujanja katika kazi, kutii kanuni na utii wa wake na waume zao na kuepuka ushawishi wa mashoga na watu wengine.

Degree

thesis:*
Level dc:type.qualificationlevel
masters
Grantor dc:publisher.institution
The Open University Of Tanzania
Year dc:date.issued
2015

Author and committee

dc:creator, dc:contributor.*
Author dc:creator
  • Mzee, Mwanaika Madi

Subjects

dc:subject × 1

Rights

Language dc:language
en

Chain of custody

source
Harvested from
Open University of Tanzania
Base URL
repository.out.ac.tz/cgi/oai2
Last updated
2026-07-24
Source record
OAI-PMH GetRecord
citation

Mzee, Mwanaika Madi. Kuchambuwa Maudhui ya Hadithi za Watoto Katika Jamii ya Wapemba. masters thesis, The Open University Of Tanzania, 2015.