Back to results

The Open University Of Tanzania

Uchambuzi wa Viangama Katika Kiswahili cha Mazungumzo Unguja

Abstract

dc:description.abstract

Utafiti huu unaohusu uchambuzi wa viangama katika Kiswahili cha mazungumzo lengo lake kuu ni kuchambua viangama katika Kiswahili cha mazungumzo Unguja. Utafiti huu umeongozwa na nadharia ya viangama ya Zwicky (1977) amechambua viangama sahili, viangama maalumu na viangama funge. Utafiti umetumia mbinu mbalimbali katika ukusanyaji wa data zake. Utafiti umefanyika Unguja mjini katika shehia nne ambazo ni Shangani, Mchangani, Mwanakwerekwe na Mombasa. Walengwa wa utafiti huu ni wazee, watu wa makamo na vijana. Kila shehia wamesailiwa watu 25 wa umri na jinsia tafauti na kufanyiwa usaili watu 100.. Utafiti huu umetumia mbinu za hojaji, usaili na ushuhudiaji. Utafiti umetumia data simulizi ambapo mtafiti amefanya usaili na kushuhudia kwa kusikiliza mazungumzo kutoka mikusanyiko ya watu mbalimbali. Kwa upande wa uchambuzi wa data, mtafiti amechambua aina za viangama tamati zilizomo katika Kiswahili cha mazungumzo, maumbo ya viangama tamati katika Kiswahili cha mazungumzo na kategoria za maneno ambazo ni viegemewa vya viangama tamati katika Kiswahili cha mazungumzo. Kwa upande wa matokeo ya utafiti, data zimeonesha kuwa Kiswahili cha mazungumzo kina viangama tamati vyenye maumbo yafuatayo: viwakilishi, vimilikishi, viulizi, vivumishi, viunganishi na vielezi. Maumbo hayo yameegemezwa kwenye nomino, vitenzi, vielezi na viwakilishi. Kwa upande wa mapendekezo mtafiti amependekeza ufanyike utafiti wa Kiswahili cha mazungumzo Unguja na lahaja ya Kipemba. Pia anapendekeza ufanyike utafiti wa viangama awali katika Kiswahili cha mazungumzo. Vile vile amependekeza ufanye utafiti linganishi baina ya Kiswahili cha mazungumzo na lugha za Kibantu. Mwisho amependekeza ufanywe utafiti wa viangama awali vya Kiswahili sanifu.

Degree

thesis:*
Level dc:type.qualificationlevel
masters
Grantor dc:publisher.institution
The Open University Of Tanzania
Year dc:date.issued
2015

Author and committee

dc:creator, dc:contributor.*
Author dc:creator
  • Makame , Mussa Khamis

Subjects

dc:subject × 1

Rights

Language dc:language
en

Chain of custody

source
Harvested from
Open University of Tanzania
Base URL
repository.out.ac.tz/cgi/oai2
Last updated
2026-07-24
Source record
OAI-PMH GetRecord
citation

Makame , Mussa Khamis. Uchambuzi wa Viangama Katika Kiswahili cha Mazungumzo Unguja. masters thesis, The Open University Of Tanzania, 2015.