Back to search

The Open University of Tanzania

Kufuwawa kwa Miiko na Kupotoka kwa Maadili Uchunguzi Kifani wa Jamii ya Wabungu

Abstract

dc:description.abstract

Lengo kuu la utafiti huu lilikuwa ni kuchunguza na kutafuta miiko ya jamii ya Wabungu. Mada ya utafiti ilikuwa ni kufuwawa kwa miiko na kupotoka kwa maadili uchunguzi kifani kwa jamii ya Wabungu. Mtafiti alitumiya njia ya uchunguzi kifani ili kumwezesha kupata data alizozikusudiya. Njia hii ilimwezesha mtafiti kuwasaili watafitiwa wakati huo huo akifanya uchunguzi. Ukweli ni kwamba katika utafiti huu, mtafiti aliongozwa na nadharia za Elimu ina Kwao na Fasihi ina Kwao pamoja na nadharia ya Kila Jamii ina Ujumi Wake. Kwa hali hiyo utafiti ulikuwa umesanifiwa vizuri na kumwezesha kupata data za awali na za msingi kwa wakati. Jumla ya watafitiwa 23 walisailiwa. Kati ya hawa wanaume walikuwa 15 na wanawake 8 tu. Katika utafiti huu mtafiti aliweza kukusanya miiko takribani 114 kati ya miiko hiyo yote ni miiko 20 tu ndiyo iliyojadiliwa kwa kiwango cha maadili na mingine ilijadiliwa kifalsafa na miiko mingine iliorodheshwa tu. Baada ya uchambuzi wa data zote za maelezo mtafiti alibaini kuwa ni kweli kuwa maadili ya jamii ya Wabungu yamepotoka. Watafitiwa walimweleza mtafiti usasa ni chimbuko kuu la kupotoka kwa maadili. Usasa huo ni pamoja na elimu isiyokuwa na misingi ya maadili mema na ujumi wa jamii inayowazunguka. Aidha taalimu ina kwao na fasihi ina kwao ilishadidia kupotoka kwa maadili katika jamii ya Wabungu. Mwisho mtafiti alitowa mapendekezo kwa Wizara husika kama Elimu na Utamaduni kuliangalia suala hilo kwa mtazamo wa kufuwawa kwa miiko na maadili. Pia tafiti nyingi iwezekanavyo zifanywe ili jamii za Kitanzania ziweze kuuhisha miiko ambayo ni nyanja adhimu katika sanaajadiiya.

Degree

thesis:*
Level dc:type.qualificationlevel
masters
Grantor dc:publisher.institution
The Open University of Tanzania
Year dc:date.issued
2013

Author and committee

dc:creator, dc:contributor.*
Author dc:creator
  • Kisanji, Joachim Aloyce Ndamba

Subjects

dc:subject × 1

Rights

Language dc:language
en

Chain of custody

source
Harvested from
Open University of Tanzania
Base URL
repository.out.ac.tz/cgi/oai2
Last updated
2026-07-24
Source record
OAI-PMH GetRecord
citation

Kisanji, Joachim Aloyce Ndamba. Kufuwawa kwa Miiko na Kupotoka kwa Maadili Uchunguzi Kifani wa Jamii ya Wabungu. masters thesis, The Open University of Tanzania, 2013.