Back to search

The Open University of Tanzania

Athari za Itikadi katika Nyimbo za Harusi za Kizanzibari

Abstract

dc:description.abstract

Utafiti huu unahusu Athari za Itikadi katika nyimbo za Harusi za Kizanzibari. Utafiti ulifanyika katika visiwa vya Unguja na Pemba. Kwa upande wa kisiwa cha Unguja, utafiti ulifanyika katika Mkoa wa Mjini Magharibi, Wilaya ya Magharibi katika shehia za Mwanyanya na Mfenesini. Kwa upande wa kisiwa cha Pemba, utafiti ulifanyika katika Mkoa wa Kusini, Wilaya ya Chake Chake katika shehia ya Tibirinzi. Utafiti ulitumia mbinu ya usaili na ushiriki ambapo watoa taarifa 40, wanawake wenye umri kati ya miaka 20 – 60 walitumika katika kutoa data zilizokamilisha utafiti huu. Katika ukusanyaji na uchambuzi wa data, njia iliyotumika ni njia ya maelezo, kwani ndiyo muafaka kwa utafiti huu. Utafiti umegundua kuwa, nyimbo za harusi za Kizanzibari, huimbwa katika miktadha tafauti, kama vile, wakati wa kuwekwa ndani mwari harusi, kwa ajili ya mafunzo na matayarisho ya harusi, wakati wa kwenda kuowa, wakati wa kurudi na bibi harusi, tukitaja kwa uchache. Aidha, utafiti umegundua kuwa, nyimbo za harusi za Kizanzibari zimebeba itikadi nyingi, kama vile, itikadi juu ya umuhimu wa utii, umuhimu wa kuwa msafi, umuhimu wa kuheshimu ndowa, umuhimu wa mashirikiano, na itikadi juu ya umuhimu wa kuwa na uvumilivu katika ndowa, tukitaja kwa uchache tu.Aidha, utafiti huu umegundua kuwa matumizi ya lugha katika nyimbo za harusi za Kizanzibari, ni muhimu katika kuzifanya nyimbo zifahamike kwa wanandoa.

Degree

thesis:*
Level dc:type.qualificationlevel
masters
Grantor dc:publisher.institution
The Open University of Tanzania
Year dc:date.issued
2016

Author and committee

dc:creator, dc:contributor.*
Author dc:creator
  • Abdulla, Layla Msabah

Subjects

dc:subject × 1

Rights

Language dc:language
en

Chain of custody

source
Harvested from
Open University of Tanzania
Base URL
repository.out.ac.tz/cgi/oai2
Last updated
2026-07-24
Source record
OAI-PMH GetRecord
citation

Abdulla, Layla Msabah. Athari za Itikadi katika Nyimbo za Harusi za Kizanzibari. masters thesis, The Open University of Tanzania, 2016.