Back to search

The Open University Of Tanzania

Kuchunguza Matumizi ya Lugha katika Riwaya ya Kiswahili: Uchunguzi Kifani wa Vipuli vya Figo na Siri za Maisha

Abstract

dc:description.abstract

Riwaya za Vipuli vya Figo na Siri za Maisha ni riwaya mpya, kwa maana ya riwaya za karibuni zenye kusheheni matukio ya kusisimua na kutoa mafunzo kwa yeyote aliyewahi ama atakayezisoma aidha kwa kujiburudisha au kujifunza. Ni kazi nzuri na za kuvutia za Profesa Emmanuel Mbogo. Utafiti huu ulifanywa kwa lengo la kuchunguza matumizi ya lugha katika riwaya hizi mbili na kuibua dhamira mbalimbali zilizojitokeza. Utafiti huu ulikuwa na malengo mahususi matatu ambayo ni, kuchambua matumizi ya lugha ya kitamathali katika riwaya za Vipuli vya Figo na Siri za Maisha, kuchambua matumizi ya lugha yasiyo ya kitamathali katika riwaya za Vipuli vya Figo na Siri za Maisha na kuwasilisha dhamira zinazojitokeza katika riwaya za Vipuli vya Figo na Siri za Maisha. Katika kutimiza malengo haya, tulikusanya data kwa kutumia mbinu za usomaji makini na upitiaji wa nyaraka maktabani na kufanya uchambuzi wa data kwa kutumia mbinu ya mkabala wa kimaelezo na nadharia ya Simiotiki. Maokeo ya utafiti yanaonyesha kwamba, matumizi ya lugha yaliyojitokeza katika riwaya za Vipuli vya Figo na Siri za Maisha ni tamathali za usemi na zisizo tamathali za usemi. Matumizi ya lugha ya kitamathali ni tashibiha, tashihisi, tafsida, sitiari, kejeli na dhihaka. Matumizi ya lugha yasiyokuwa ya kitamathali ni misemo, nahau, takriri, tanakali sauti na taharuki. Pamoja na matumizi haya ya lugha ya kitamathali na yasiyokuwa ya kitamathali pia kuna dhamira mbalimbali zimejitokeza katika riwaya tafitiwa. Dhamira hizo ni biashara haramu, umuhimu wa elimu katika jamii, Dhamira ya malezi katika jamii, hali ngumu ya maisha, siasa na uchumi na nafasi ya mwanamke katika jamii.

Degree

thesis:*
Level dc:type.qualificationlevel
masters
Grantor dc:publisher.institution
The Open University Of Tanzania
Year dc:date.issued
2015

Author and committee

dc:creator, dc:contributor.*
Author dc:creator
  • Kimambo, Sidora Joseph

Subjects

dc:subject × 1

Rights

Language dc:language
en

Chain of custody

source
Harvested from
Open University of Tanzania
Base URL
repository.out.ac.tz/cgi/oai2
Last updated
2026-07-24
Source record
OAI-PMH GetRecord
citation

Kimambo, Sidora Joseph. Kuchunguza Matumizi ya Lugha katika Riwaya ya Kiswahili: Uchunguzi Kifani wa Vipuli vya Figo na Siri za Maisha. masters thesis, The Open University Of Tanzania, 2015.