Back to search

The Open University Of Tanzania

Ufasihi Simulizi katika Riwaya za Shaaban Robert: Mifano kutoka Adili na Nduguze na Wasifu wa Siti Binti Saad

Abstract

dc:description.abstract

Utafiti huu unahusu ufasihi simulizi katika riwaya za Shaaban Robert kwa kutumia mifano ya riwaya: Mfano kutoka Adili na Nduguze na Wasifu wa Siti Binti Saad. Lengo kuu la utafiti huu lilikuwa ni kufafanua vipengele vinavyojenga fasihi simulizi na jinsi vilivyotumika kuibua dhamira, na kutathmini na kubaini jinsi mtunzi huyo anavyofumbata mbinu ya mwingilianomatini katika kazi zake za fasihi, na namna mbinu hizo zinavyotumika kuibua dhamira za riwaya hizo. Sampuli ya utafiti huu iliteuliwa kwa kutumia mbinu ya uteuzi wa madhumuni maalumu, nasibu na ile ya uteuzi rahisi, wakati ambapo data zilikusanywa kwa kutumia mbinu nne, ambazo ni mapitio ya maandiko, usaili, dodoso na majadiliano ya vikundi. Uchambuzi wa data ulifanyika kwa kutumia mbinu ya uchambuzi maudhui. Aidha nadharia ya mwingilianomatini ilitumika kukusanyia, kuchambua na kujadili data za utafiti huu. Matokeo ya utafiti huu yameonesha kuwa, mtunzi ametumia mbinu ya mwingilianomatini katika utunzi wake, pamoja na kuwa kazi hizo zina mpishano katika kutungwa kwake. Aidha, riwaya zote mbili ni matokeo ya athari za mapokeo ya matumizi ya fasihi simulizi ya Kiafrika, ambapo mtunzi ameathiriwa na masimulizi ya hadithi za fasihi simulizi na masimulizi ya kawaida katika utunzi wa riwaya ya Adili na Nduguze na Wasifu wa Siti Binti Saad.

Degree

thesis:*
Level dc:type.qualificationlevel
masters
Grantor dc:publisher.institution
The Open University Of Tanzania
Year dc:date.issued
2015

Author and committee

dc:creator, dc:contributor.*
Author dc:creator
  • Saleh, Khatib Khamis

Subjects

dc:subject × 1

Rights

Language dc:language
en

Chain of custody

source
Harvested from
Open University of Tanzania
Base URL
repository.out.ac.tz/cgi/oai2
Last updated
2026-07-24
Source record
OAI-PMH GetRecord
citation

Saleh, Khatib Khamis. Ufasihi Simulizi katika Riwaya za Shaaban Robert: Mifano kutoka Adili na Nduguze na Wasifu wa Siti Binti Saad. masters thesis, The Open University Of Tanzania, 2015.