Back to search

The Open University Of Tanzania

Kuchunguza dhima za vitendawili vya jamii ya Wanyisanzu wa Iramba, Singida, Tanzania

Abstract

dc:description.abstract

Lengo kuu la utafiti huu lilikuwa ni Kuchunguza dhima za vitendawili vya jamii ya Wanyisanzu wa Iramba, Singida, kabla na baada ya uhuru wa Tanganyika, 1961. Aidha, utafiti ulitaka kujua dhima za vitendawili vya jamii ya Wanyisanzu, na kuchunguza vipengele vya fani vilivyosababishwa na mabadiliko ya kutega vitendawili katika jamii ya Wanyisanzu. Utalii wa kazi tangulizi uliongozwa na nadharia ya kuchunguza dhima za vitendawili katika jamii ya Wanyisanzu. Utafiti umetumia mbinu ya ushiriki, mahojiano, maswali ya hojaji na utalii wa nyaraka zilizotumika kukusanyia data za utafiti.Aidha, mbinu ya uchambuzi wa kimaelezo ndiyo iliyotumika katika uchambuzi wa data. Eneo la utafiti lilikuwa ni Nkata ya Nkinto na Mwangeza, wilaya ya Iramba, mkoa wa Singida. Matokeo ya utafiti yamebainisha kushuka kwa dhima za vitendawili katika jamii ya Wanyisanzu.Chanzo cha kushuka kwa dhima ya vitendawili ni; Mabadiliko ya kisomo shuleni, yamesababisha matumizi makubwa zaidi ya lugha ya Kiswahili na kusahaulika kwa lugha za asili zilizotumika, kutegea na kutegulia vitendawili. Pili, Mabadiliko ya shughuli za kiuchumi kama vile, biashara na kilimo, zimesababisha watu kutokukusanyika pamoja saa za jioni. Mwisho, kuibuka kwa ugeni wa tekinolojia (utunduizi), kumeleta mabadiliko, siyo ya kuhifadhi vitendawili kwenye maandishi, Mitandao-CD na flashi.

Degree

thesis:*
Level dc:type.qualificationlevel
masters
Grantor dc:publisher.institution
The Open University Of Tanzania
Year dc:date.issued
2015

Author and committee

dc:creator, dc:contributor.*
Author dc:creator
  • Damka, Amos Ben

Subjects

dc:subject × 1

Rights

Language dc:language
en

Chain of custody

source
Harvested from
Open University of Tanzania
Base URL
repository.out.ac.tz/cgi/oai2
Last updated
2026-07-24
Source record
OAI-PMH GetRecord
citation

Damka, Amos Ben. Kuchunguza dhima za vitendawili vya jamii ya Wanyisanzu wa Iramba, Singida, Tanzania. masters thesis, The Open University Of Tanzania, 2015.